Saturday, January 28, 2017

Serikali ya Syria yakana kuwa Bashar al Assad anaugua

Serikali ya Syria imekana taarifa kuwa Rais Bashar al-Assad anaugua, ikisema ni uvumi mtupu unaotumiwa na maadui wa Assad kujaribu kuwapa motisha wanamgambo na waasi waliokata tamaa. Akisisitiza kuwa Asaad yu buhari wa afya na kwamba anaendelea na kazi zake kawaida, Wameshtumu wapinzani kwa kile wanachokitaja kuwa kutumia propaganda. Waasi hao wamedaiwa kueneza taarifa ghushi kwamba Bashar amepata mshutuko wa moyo au ana maradhi ya kiakili baada ya miaka sita ya vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.

0 comments:

Post a Comment